CHAMA CHA UZALENDO CHA TISHIA KUJIONDOA KATIKA MUUNGANO WA AZIMIO
Taarifa yake ,Caroline Katana
Chama Cha Uzalendo C C U kimetishia kujiondoa katika muungano wa Azimio na kujiunga na chama cha Wiper ili kumpa nafasi kinara wa muungano huo Raila Odinga kujiunga na serikali ya Kenya Kwanza ili kuendeleza mazungumzo ya kutatua changamoto msingi zinazolikumba taifa la Kenya .
Hii ni baada ya chama cha Uzalendo kujitenga na mazungumzo ya kitaifa yanayopangwa na srikali ya Kenya Kwanza .
Kinara wa CCU Richard Onsongo amesema kwamba kinara wa Azimio Raila Odinga anajipendekeza katika serikali ya Kenya Kwanza ili apate kutengeza nafasi za vyeo katika serikali hio swala ambalo hawaliungi mkono.
Aidha amesema kwamba kuna haja ya rais Wiliam Ruto kubeba msalaba wake wenyewe katika maswala ya utatuzi wa changamoto zinazolikumba taifa pasi na kuisurutisha mirengo mingine ya kisiasa.
“ Hatutaki kuungana na kinara wa azimio Raila Odinga na ODM yake kuhusu mambo ya mazungumzo na uiyano , rais Ruto ana manifesto yake aliyosimama nayo wakati wa kampeni na alisema anaweza kusimamia nchi ,acha asimamie nchi yake ikimshinda imshinde mwenyewe ,ikiwa nzuri ni sawa ,ikileta shida kama vile inavyoendelea kushuhudiwa hilo ni tatizo lake mwenyewe ,” Asema bw.Onsongo .
Mwenyekiti wa chama cha CCU kaunti ya Kisii Dennis Samson Omwenga amesema kwamba chama cha CCU kitasimama na wananchi ili kuhakikisha matakwa yao yanatekelezwa na serikali ya Kenya Kwanza .
“ Sisi tutakuwa firimbi ya wananchi kama nembo ya chama chetu inavyoashiria ,chochote kile ambacho kinaenda kombo katika serikali ya Kenya Kwanza tutapiga firimbi na tuambie wananchi , kwa sasa hakuna haja ya mazungumzo ila wapewe muda wakutekeleza manifesto yao kwa wananchi ,” Asema bw Omwenga .
Aidha amesisitiza kuwa taifa la kenya lina hitaji amani ,upendo na umoja japo kusema kuwa chama cha CCU hakiwezi kuunga mkono serikali yenye manifesto yake .
“Naunga mkono vijana wa Gen Z wanavyopigania haki ya wakenya japo nawaomba kutulia na kumpa rais Wiliam Ruto kutekeleza manifesto yake mana kwa sasa tuko nusu ya kipindi chake cha uongozi kwa hio tumpe muda wa mwaka mmoja Zaidi ,endapo ata feli basi Gen Z warudi barabarani kutafuta haki ya wakenya ,”Asisitiza bw Omwenga .
Kwa upande wake Pauline Wanja Kamau mwanachama wa CCU amemtaka rais Ruto kuhakikisha vijana waliokamatwa wakati wa maandamano kuachiliwa huru .
“ Ni uchungu kuona vijana wadogo wakiuwawa katika maandamano ya kutetea haki ya wakenya ,tunaomba rais Ruto ahakikishe hawa vijana wanaachiliwa huru ,ni uchungu kuona vijana wakitekwa nyara wakipigania haki sisi kama chama cha Uzalendo hatutaruhusu unyama huo kuendelea ,” Asema bi Kamau .
Hata hivyo C C U ikishikilia kuwa ni sharti serikali ya kenya kwanza kuhakikisha wafisadi serikalini wanatolewa afisini ili kutoa nasafi ya uchunguzi hadi pale watakapothibitishwa kuwa wasafi na taasisi husika , kuchunguza ubadhirifu wa fedha katika hazina ya NG-CDF na kuhakikisha fedha za basari zitumwa shuleni moja kwa moja .
Aidha kimeshikilia kwamba hakuna haja ya mazungumzo ya kitaifa kufanyika ili kuleta suluhu la changamoto msingi zinazolikabili taifa .
Chama cha Uzalendo kilichoanzishwa mwaka wa 2005 hadi sasa kiko na wanachama 600,000 katika kaunti 24 za humu nchini .


Comments
Post a Comment