VITA YA MAZENSE NA MABIBO KUAMULIWA KESHO KINESI.
Bondia Roja Mjeshi wa kwanza kulia huku kushoto kwake Mpinzani wake Said Macho wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kumalizika zoezi la kupima uzito Lililofanyika Uwanja wa Las Vegas Mabibo Mahakama ya Ndizi Jijini Dar es salaam leo Novemba 19,2022 wakijindaa na Pambano La "Dar Boxing Derby " linalotarajiwa kufanyika Novemba 20,2022 Uwanja wa Kinesi Dar es salaam Na.Khadija Seif Tz MABONDIA wapewa fursa tena Msimu wa tatu wa Pambano la "Dar boxing derby " kesho Novemba 20,2022 huku Mabondia wahaidi kufanya vizuri ili kuleta hamasa kwa waandaaji (Peaktime)kuendelea kuwakumbuka na kuwapa nafasi Mabondia chipukizi. "Tumeonyesha njia kwenye Mapambano makubwa na sasa tunachukua furusai ya kuwapa nafasi Mabondia wadogo wenye vipaji ili wakajaze nafasi za mabondia ambao wamemaliza muda wao ( wastaafu ). Pambano la boxing derby" kwa zaidi ya Msimu wa tatu mahususi kwa mabondia wenye vipaji vichanga na vipya kwa Ji...