SHULE YA MSINGI YA WAA YANG’AA KIMAZINGIRA KUPITIA UFADHILI WA VYOO KUTOKA KWA KAMPUNI YA MOZZART BET KWA USHIRIKIANO NA WAKFU WA RASHID ABDALLAH .

 

Usimamizi wa kampuni ya Mozart bet pamoja na wadau mbalimbali.

Wakfu wa  Rashid  Abdallah  umeukabidhi  rasmi  usmimamizi  wa shule ya msingi ya Waa  mradi wa vyoo  18, madawati 100, sodo miongoni mwa pembejeo zenginezo  za elimu ,  kupitia ufadhili wa kampuni ya ubashiri ya Mozatt bet  uliogharimu  takriban shilingi million 3.4.

Hatua hio imejiri  kufuatia hali mbaya ya vyoo iliyokuwa ikishuhudiwa shuleni  humo iliyohofiwa kusababisha mikurupuko  ya maradhi yanayotokana na mazingira chafu.

Mkurugenzi mkuu wa mozzart bet nchini Kenya  SaS'a  Krneta.

MkMkurugenzi  wa kampuni hio ya Mozzart bet nchini kenya Sas’a Krneta amesema kwamba mazingira bora ya vyoo  utaimarisha hali ya usafi shuleni humo na kuhakikisha usalama wa kiafya kwa wanafunzi na walimu .

“ Tumewakabidhi vyoo kumi na 18 ,saba  vitatumika na wanafunzi wakiume  vyengine saba  viwasaidia wanafunzi wakike huku vyoo vine vitatumika na walimu ,nina imani hatua hii itachangia afya bora na kuimarika kwa viwango vya elimu miongoni mwa wanafunzi ,”Asema bw.Krneta .

Kadhalka  mkurugenzi huyo ameahidi kuendeleza mpango wa kuzisaidia jamii kaunti ya Kwale kupitia miradi mbalimbali  ili kuimarisha hali zao za maisha .

“Sio mara yangu ya kwanza  kufika katika eneo hili na nina matumaini ya kurudi tena mwaka ujao ili kutathmini maendeleo ya elimu ya wanafunzi wa shule hii ,nahitaji kujua endapo mradi huu utakuwa na manufaa kwa wanafunzi ,ili tuweze kuanzisha mpango mbadala wa kusaidia jamii na miradi sawia ,”Adokeza bw Krneta .

Hata hivyo ameelezea umuhimu wa kampuni hio ya Mozzart bet kushirikiana na wakfu wa Rashid Abdallah ili kuzisaidia jamii kaunti ya Kwale .

 “Kufikia sasa tumefadhili Rashid Abdallah Super Cup kama njiamojawapo ya kukuza vipaji  vya vijana  katika nyanja ya soccer katika  eneo hili  na  leo tumefanikisha mradi wetu wa kwanza katika sekta ya  elimu  na hatutakomea hapa tutaendelea kuzisaidia jamii nchini kenya ,” Asema bw Krneta.

                      Mwanzilishi wa wakfu wa Rashid Abdullah,  Rashid Abdullah.

Mwanzilishi wa wakfu wa Rashid Abdallah ,Rashid Abdallah amehoji kwamba mazingira bora ndio nguzo kuu ya afya njema kwa jamii .

“Jamii ikiwa salama kiafya ni ishara kwamba hata vizazi vijavyo zitakuwa salama ,ni pongeze kampuni ya Mozzart bet  kwa kujua thamani ya watoto wetu ,mana wasichana wanapokuwa katika hedhi wanapitia mazingira magumu endapo  vyoo haviko katika hali nzuri na pia huchangia mikurupuko ya maradhi ,lakini vyoo vikiwa salama inamaanisha utulivu wa akili na tunatarajia  kutapa matokeo bora ya mitihani inayokuja  ,” Asema bwa Rashid 

Wakati uohuo bw.Rashid ametoa chanagamoto kwa wafadhili zaidi kujitokeza  na kupiga jeki juhudi za wakfu huo  ili miradi sawia na hio iweze kuwafaidi wanafunzi Zaidi katika shule mbalimbali eneo la Matuga. 

Akigusia swala la Rashid Super Cup ,mwanizlishi huyo ameafiki maandalizi ya dimba la tano eneo la Matuga yanaendelea ,dimba  linalorajiwa kuanza mwezi wa Agosti  .

“Mozzart bet  wameonyesha nia kuwa wanatuthamini ,kutufadhili kwa  misimu miwili tulieka historia kwa mara ya kwanza kwa  kupata mchezaji kutoka ligi ya  chini kusajiliwa moja kwa moja katika ligi kuu nchini Kenya ,hatuangalii peza zinazotolewa kwa mshindi lakini jinsi anavyojitolea kufadhili vifaa vya michezo ,maandalizi ya dimba hilo ,kwa hio tuna matuimani kuwa safari hii mozzart atakuja akiwa amejipanga hata Zaidi ,”Adokeza bw Rashid.

Vivian Moraa wa Miss Universe Kenya ametoa changamoto kwa watoto wakike kaunti ya Kwale kujizatiti katika masomo  ili kuafikia ndoto zao maishani.

                           Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Waa Amina Said.

Mwalimu  mkuu wa shule ya msingi ya Waa Amina Said ameipongeza kampuni ya mozzart bet kwa kuboresha mazingira ya shule hio ,akiitaja kuwa hajua moja ya kuinua viwango vya elimu shuleni humo .

“Katika elimu tunasema kuwa mazingira safi  ni bora zaidi ,ni lazima wanafunzi tuwape mazingira mazuri ili waweze kutuliza vichwa vyao na wasome vyema ,vyoo hivi vitasaidia sana mana awali tumekuwa na changamoto ya watoto kutofika shuleni walipopatwa na michafuko ya tumbo mana hatukuwa na vyoo salama  vya kuwahifadhi vizuri mana hata maji vilikosa ,wasichana wetu pia walikuwa wakipitia changamoto walipokuwa katika hedhi ,lakini kwa sasa vyoo hivi vitatusaidia pakubwa sana katika uimarishaji wa viwango vya elimu hapa Waa kwani tunatarajia wanafunzi  wote kuhudhuria masomo bila kukosa ,”Asema bi Said .

Bi .Said akiwaomba wahisani Zaidi na serikali ya kaunti ya Kwale kujitokeza ili kuwasaidia kutanzua baadhi ya changamoto sugu zilizogira shule hio ,ikiwemo ile ya ukosefu wa ua na umeme.

Naibu gavana wa Kwale Chirema Kombo.

Hata hivyo naibu gavana wa Kwale Chirema Kombo ameipongeza kampuni ya mozzart bet na wakfu wa Rashid Abdallah  kwa kuboresha mazingira ya shule ya msingi ya Waa kupitia ujenzi wa vyoo vya kisasa  huku akiwataka wakaazi wa Kwale kutoingiza  siasa katika swala la elimu ila kuipa nafasi serikali ya Kwale kuwahudumia wanafunzi kwa usawa .

Comments

Popular posts from this blog

Kwale Doctors Strike Enters Day 3 Amid Chaos, Unpaid Salaries, and Deteriorating Healthcare Services

Lack of focus on sanitation and hygiene interventions puts children at risk of death due to bacterial infections causing diarrhea in Kilifi County.

CHAMA CHA UZALENDO CHA TISHIA KUJIONDOA KATIKA MUUNGANO WA AZIMIO