WAKAAZI ELFU 20 KAUNTI YA KWALE WAFAIDIKA NA CHAKULA CHA MSAADA KUTOKA KWA SERIKALI.
KITAIFA
Taarifa yake , Caroline Katana.
Wakaazi elfu 20 kutoka familia zisizobahatika kaunti ya Kwale ni miongoni mwa wakenya
wanaoelendelea kufaidika na chakula cha msaada kutoka kwa serikali ya kitaifa kupitia wizara ya
mipango maalum (special programs) .
Mbali na mradi wa inua jamii , wizara hio ya mipango maalum inaendeleza mradi wa utoaji chakula
kwa wajane ,watoto mayatima ,wazee ,wagonjwa na watu wanaoishi katika lindi la umaskini kote
nchini.
Akizungumza wakati wa ugavi wa chakula hicho katika wadi ya Tsimba-golini huko Matuga kaunti ya Kwale naibu msemaji katika afisi ya Rais Mwanaisha Chidzuga ,amesema kwamba hatua hio ni baadhi ya mikakati ya serikali kuhakikisha wakenya wasizojiweza wanapata lishe kama wakenya wengine .
“ Zaidi ya wakaazi elfu moja hapa wadi ya Tsimba-golini watapokea chakula ,na katika awamu hii ya
kwanza nina lenga wakaazi elfu 20 katika kaunti ya Kwale katika zoezi hili la siku tatu ,tunawapatia
ruzuku ya mchele, maharage na akinamama wenye watoto wadogo wanapokea unga wa uji ,” Asema bi
.Mwanaisha .
Bi. Mwanaisha ametumia fursa hio pia kuhamasisha umma umuhimu wa kujisali katika mpango wa
serikali wa bima ya afya ya Social Health Insuarance Fund ( SHIF) chini ya mradi wa Social Heath
Authority SHA , ili kuona kuwa wanafaidika na huduma za bure za matibabu katika hospitali za umma
kufikia mwezi Octoba ambapo mpango huo unatarajiwa kuanza rasmi .
“ Wakaazi wanatakiwa kujisali kupitia Social Health Authority SHA ,kupitia nambari ya usajili ya *147#
kinyume na hio hawatafaidika na huduma hio ya matibabu bila malipo, tunafahamu kuwa asilimia
kubwa ya akinamama Kwale wanaugua saratani ya uzazi na hawana fedha za kugharamikia matibabu
,kwa hio itakuwa afueni kwao endapo watajiunga na mpango huu wa bima hii ya afya ,”Asema bi
Mwanaisha .
Kadhalka amegusia swala la mradi wa serikali wa nyumba za bei nafuu ,akisema kwamba umetoa nafasi
nyingi za ajira kwa vijana hivyo kuwataka kujitokeza kwa wingi ili kufaidika na nafasi hizo .
“ Badala ya vijana kuketi katika maskani na kula mugukaa ,nawasihi wajitokeze kwa nafasi hizo ili
waweze kupata mapato ya kujikimu kimaisha ,vilevile tuna fahamu kwamba sherehe ya kitaifa ya
Mashujaa itafanyika katika kaunti hii ya Kwale na ninaelewa kwamba vijana wengi watahitajika ili
kufanikisha kazi mbalimbali kwa ajili ya maandalizi ya siku hio ,hivyo ni sharti vijana wetu hapa Matuga wakumbatie nafasi hizo kikamilifu ,”Aongeza bi Mwanaisha .
Wakati uohuo bi .Mwanaisha ameunga mkono hatua ya rais William Ruto ya kuvunja baraza la mawaziri ili kufanya marekebisho ,japo kumuomba Rais Ruto kuhakikisha ukanda wa pwani unapata nafasi zaidi za mawaziri katika mabadiliko yake.
“Nawasihi wakenya wamuunge mkono rais Ruto katika juhudi yake ya kulifanyia mabadiliko baraza la
mawaziri ,sisi kama wa pwani alikuwa ametupatia mawaziri wawili ila namuomba endapo nafasi zitapatikana atuongezee mawaziri pwani ,kwani mawaziri wa pwani wamekuwa wamejizatiti Zaidi katika kutekeleza majukumu yao kwa wakenya ,”Asema bi Mwanaisha .
Kwa upande wake Mwanamwita Hamisi kutoka kijiji cha Maramuni aliyepokea chakula hicho
ameipongeza hatua ya serikali ya kitaifa ya kuwasaidia wakaazi wasiojiweza .
Katika swala la usajili wa bima ya afya ya SHA , mama Mwanamwita ameutaja mradi huo kulenga
kutatua changamoto za matibabu zinazowakumba wakaazi hususan kinamama ambao kwa miongo
mingi wamekuwa wakitaabikia huduma bora za afya kufuatia hali zao za uchochole.
kupitia hali ngumu ya lishe kutokana na makali ya kiangazi yanayoshuhudiwa katika baadhi ya maeneo
kaunti ya Kwale .
“ Kuna ukame wa siri ambao unashuhudiwa katika maeneo ya Tsimba-golini na wakaazi wengi
wamekosa chakula mashambani mwao kwa miaka mingi ,tunashukru Rais wetu kwa msaada huu na
tunaomba uendelee kutolewa ili usaidie jamii zisizojiweza ,Akiri bw. Makoti.
Katika hafla hio chifu wa lokesheni ya Golini Nchangoma Mbwana ,amelitaja eneo hilo kusheheni visa
vya utovu wa usalama vinavyotekelezwa na vijana wanaoasi elimu ,akiwataka wazazi kuwajibikia
majukumu ya watoto wao na kuwafichua washukiwa wa uhalifu ili mkono wa sheria uchukue mkondo
wake na kuhakikisha jamii inaishi kwa amani na usalama .




Comments
Post a Comment