ZIARA ZA RAIS KATIKA MATAIFA YA NJE ZA CHANGIA KUKUA KWA UTALII NCHINI
Pich: washikadau wakiokota wakataka fuo ya Diani Kwale
Safari za nje za rais wa jamhuri ya kenya William Ruto zimetajwa kuwa na mchango mkubwa katika uimarishaji wa sekta ya utalii humu nchini .
Rais Ruto ametajwa kuwa mstari wa mbele kuuza utalii wa kenya katika ziara zake kote ulimwenguni.
Katibu katika wizara ya utalii nchini John Ololtwaa aliyekuwa akizungumza huko katika fuo ya bahari ya Kongo kaunti ya Kwale baada ya zoezi la kusafisha fuo ya bahari ya Diani ,amesema kuwa idadi kubwa ya watalii wanaozuru taifa hili inatokana na ushawishi wa rais Ruto anapokuwa katika mataifa ya kigeni .
“ Na rais wetu wenyewe ameweza kuinua nchi yetu na yale mambo ambayo anaongea katika mataifa ya nje na yale mambo ambayo ana fanya humu nchini ,tuko na mpango wa kuinua taifa hili huko Turkana kupitia mpango wa Kenya is Home of Origin ,” Asema katibu Ololtwaa .
Katibu huyo ameafiki kuwa wizara hio ya utalii na wanyamapori kwa ushirikiano na serikali za kaunti eneo pwani imeanzisha mchakato wa kufufua vyanzo vya utalii , ili kuwavutia watalii Zaidi eneo la pwani mwa Kenya .
“ Awali tulikutana na magavana wa pwani ili kujadili jinsi serikali za kaunti za pwani zitaweza kushirkiana na serikali ya kitaifa na wizara ya utalii na wanyamapori kuvitambua na kuviboresha vivutio vya utalii ili kuvutia wageni wengi Zaidi pwani mwa kenya ,katika kaunti ya Kwale tuko na eneo ambalo limejichora ramani ya Afrika (map of Africa ) ambalo likiboreshwa litaweza kuwavutia wageni wengi katika kila pembe ya ulimwengu ,” Ameongeza katibu Ololtwaa.
katibu katika wizara ya utalii Jonh OloltwaaKadhalka ameeleza kuwa sekta ya utalii ni mojawapo ya vitega uchumi vikuu nchini na imechangia kuimarika kwa uchumi wa nchi .
“Wale wageni wote kutoka pembe zote za ulimwengu wanaleta mapato makubwa katika kaunti hii ya K wale na taifa zima kwa ujumla kwani wamechangia kukua kwa biashara za kitalii katika eneo hili la Diani ,”Adokeza katibu Ololtwaa .
Katibu huyo akihoji kuwa wizara ya utalii inashirikiana na serikali ya kaunti ya Kwale ili kuboresha miundo msingi ikiwemo ,ukarabati wa taa za barabarani na uboreshaji wa kiwanja cha ndege cha Ukunda .
Aidha ameeleza kuwa miongoni mwa mipangilio iliyopo katika uboreshaji wa sekta ya utalii ni kuhakikisha wameshirikiana na wamiliki wa hoteli za kitalii pwani ili kuhakikisha wanaunda kanuni za maadili (code of conduct ) kwa wahudumu wa fuo ya bahari .
“ Kanuni hii itasaidia kuimarisha usalama katika fuo ya bahari pamoja na kulinda mazingira ya bahari ili kuhakikisha watalii wanaozuru fuo hio wanapata usalama wakutosha ,” Asema katibu Ololtwaa .
Wakati uohuo ametoa changamoto kwa wahudumu wa fuo ya bahari kuungana na kuanzisha chama cha ushirika ili waweze kufaidika na mikopo kutoka kwa serikali ili waweze kujiendeleza kiuchumi .
Kwa upande wake waziri wa utalii kaunti ya Kwale Michael Mutua, amesema kwamba serikali ya kaunti inajiandaa kuja na pendekezo la mfumo wa usimamizi wa fuo ya bahari ya Diani kupitia mswada wa usimamizi wa fuo ya bahari (beach management bill).
“ Mswada huu utawasilishwa katika maeneo ya mashinani ili wananchi watoe maoni ya jinsi usimamizi wa fuo ya bahari utakavyotekelezwa ili kuiboresha zaidi fuo hio ,”Asema waziri Mutua.
Aidha amethibitisha kuwa kaunti ya Kwale itakuwa mwenyeji wa sherehe ya kuteua fuo bora za bahari na mahoteli barani Afrika na ulimwenguni mnamo tarehe 18 mwezi wa Octoba mwaka huu katika eneo la Diani .
“Siku zote sherehe hizo hufanyika nje ya bara Afrika ama ndani ya Africa katika taifa la south Africa na Egypt ,lakini mwaka huu itafanyika hapa Diani ,hivyo nawasihi wenyeji na wageni mnaozuru fuo ya Diani mdumishe usafi ,” Ameongeza waziri Mutua.
Kamishna wa Kaunti ya Kwale Stephen Orinde
Hata hivyo amesema kwamba serikali ya Kwale imeanzisha mikakati ya kukarabati taa za barabarani kutoka eneo la Carrefour hadi fuo ya bahari ya Kongo ili kuhakikisha usalama pamoja na kutoa nafasi kwa wafanyibiashara kuendeleza shughuli zao usiku na mchana .
Hata hivyo kamishna wa kaunti ya Kwale Stephen Orinde amewataka wakaazi kuwafichua vijana wanaojihusisha na visa vya utovu wa usalama ili wakabiliwe kisheria ,akiutaja ukosefu wa usalama kuwa adui mkubwa wa maendeleo .
Katika zoezi hilo la ukotaji taka katika fuo ya bahari ya Diani la kilomita 4 liliwezesha wadau walioshiriki kukusanya takriban kilo 800 za taka .



Comments
Post a Comment