FUO YA BAHARI YA DIANI YANG’AA KWA MARA YA NANE AFRIKA.

Tuzo za dunia  za tuzo za Afrika 2024

Taarifa yake : Caroline Katana. 

Taifa  la  Kenya linakila sababu ya kusherehekea  baada ya fuo ya bahari ya Diani  kutambulika tena  kama eneo la fukwe bora Zaidi  linaloongoza  barani  Afrika  katika   tuzo za dunia za tuzo za afrika za 2024 ( World Travel  Awards  ,Africa  Gala  Ceremony 2024)   iliyofanyika  katika ukumbi  wa sherehe  wa Diamonds Leisure Beach and Golf Resort, Diani , Kenya.

 Hii  ikiwa ni mara ya  nane  kwa fukwe hio ya Diani  kutambulika  kwa ubora  wake ,hivyo kuimarisha  mvuto wake  kwa wageni  wakimataifa  na wa ndani.

Hafla hio imewaleta  pamoja  viongozi  na wabunifu kutoka  bara zima la Afrika ,mashirika  ya usafiri  yaliyoweka viwango vipya vya ubora na uvumbuzi katika sekta hio ya utalii.

Gavana wa Kwale Fatuma Achani na waziri wa utalii Michael Mutua.

Gavana wa Kwale Fatuma Achani aliyehudhuria sherehe hio  amesema  kuwa  ushindi wa fukwe hio, baadhi ya hoteli  za kitalii  na uwanja wa ndege wa Ukunda  kusini mwa pwani umechochewa na ushirikiano bora kati ya serikali  kuu ,ile ya kaunti  na waekezaji  katika sekta  ya utalii.

“Tumehakikisha  fukwe yetu inasalia kuwa safi pamoja na kuimarisha usalama wa wageni na wenyeji wanaozuru fuo hiii  ya Diani , tumeeka taa za  barabarani  ,tumefungua  barabara zinazoshuka fuoni ,na kwa sasa hivi kupanuka kwa uwanja wa ndege wa Ukunda na  ufunguzi wa barabara ya Dongo-kundu kumechangia pakubwa kuimarika kwa utalii kusini mwa pwani ,”Asema gavana Achani.

Aidha amedokeza kuwa hatua hio ni ishara tosha kuwa kaunti ya kwale sasa imefunguka  katika maswala ya uekezaji na biashara mbali na  utalii.

Kadhalka kiongozi huyo akihoji kuwa ataendelea kuboresha miji ya kaunti hio ili kuhakikisha maendeleo endelevu  kwa wananchi wake.

“ Miji yetu sasa iko katika kiwango cha  manuspaa   ,Kwale ,Kinango na Diani  na Lungalunga ,katika ile mipangilio yetu yakifedha tutahakikisha kuwa tunaendelea kudumisha usafi na uboreshaji wa miji hio  ili kuzidi kufungua  nafasi za uekezaji na  kibiashara ,”Asema gavana Achani .

Gavana Achani  aidha  akisema kuwa kutambulika kwa fuo ya Diani ,hoteli za kitalii na uwanja wa ndege wa Ukunda, barani Afrika ni ishara ya kuwavutia watalii wengi Zaidi wa ndani na wale wa nje hivyo kufungua nafasi za ajira kwa vijana pamoja na kuimarisha ushuru wa kaunti hii.

Sara Rosso -Cipolini ,rais wa planhotel and hospitality group.

Rais  wa planhotel hospitality group  Sara Rosso –Cipolini  amesema kuwa sherehe hio ina umuhimu mkubwa katika sekta ya utalii kote ulimwenguni .

Aidha ameeleza kuwa sekta hio ya ukarimu ( hospitality ) kwa takriban miaka  kumi na tano  imekuwa ikipata hadi tuzo Arobaini na tano kila mwaka hatua ambayo imekuwa ya faida kubwa katika sekta ya utalii.

Meneja mkuu wa hoteli ya  Diamonds leisure beach and golf resort Andrew  Cook  ameelezea fahari  yake ya kuandaa hafla hio ya kifahari ,akisema kuwa ni sherehe muhimu kwa hoteli hio na  sekta ya ukarimu inayokua  nchini Kenya.

Andrew Cook ,meneja mkuu hoteli ya Diamonds leisure beach and golf resort.

Bw. Cook akielezea kufurahishwa kwake kwa hoteli hio kuwa miongoni mwa hoteli za kitalii zilizotambulika kwa ubora wake barani Afrika.

Angama Amboseli  ,nyumba ya kulala wageni yenye hema nzuri iliyo katika eneo la Kimana Sanctuary nchini Kenya ilitmbulika  kama  hoteli mpya inayoongoza Afrika.

Joan Ndung'u ,meneja wa kitengo cha makazi katika hoteli ya Leopard beach resort and spa.

Meneja  wa hoteli ya kitalii  Leopard  beach resort and spa  katika kitengo cha makazi  Joan Ndung’u  hakuficha  tabasamu lake baada  hoteli hio kupata tuzo kwa mara ya tatu mfululizo .

“Tulituzwa mwaka 2022 /23 na mwaka huu wa 2024 pia tumetuzwa kwa mara nyingine kwa kuwa African leading beach resort na hii ina umuhimu mkubwa sana kwetu na wageni wanaozuru hoteli yetu ,”Asema bi .Ndung’u.

Bi.Ndung’u akisema kwamba tuzo hio imewapa changamoto ya kuendelea  kuboresha bidhaa zao ili kuhakikisha mahitaji ya  wageni yanaafikiwa kikamilifu .

Kadhalka ameipongeza serikali ya kaunti ya Kwale kwa kuwapa nafasi nzuri ya kufanikisha shughuli zao za kitalii hatua ambayo imepelekea wenyeji kupata nafasi za  ajira pamoja na kuimarika  kwa biashara eneo la Diani .

Mji mkuu wa Nairobi  ulitunukiwa maeneo yanayoongoza  kwa kusafiri  kibiashara  Afrika huku klabu ya safari  ya  kifahari  ya Fairmont mountain  Kenya ilipata sifa ya  African’s leading hotel ,Somerset Westview mjini Nairobi  ikitunukiwa kama ghorofa zinazoongoza Afrika .

Katika sekta ya usafiri wa anga ,shirika la ndege la Kenya Airways lilipaa sana na kutwaa tuzo za Africa’s leading Airline na Africa’s leading airline-business class ,uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta wa Nairobi ulizidisha sifa za usafiri  wa anga  kwa kupigiwa kura ya uwanja wa ndege unaoongoza Afrika .

Mji wa pwani wa Durban uliendelea kupaa kama kivutio cha juu cha biashara ,na kupata jina la mikutano inayoongoza Afrika  ,wakati huo huo bandari ya Cape Town ilitambulika kama bandari ya kuongoza  kwa  safari za baharini barani Afrika ,ushuhuda  wakuongezeka kwa umuhimu wake katika sekta ya bahari na utalii .

Tanzania illibuka  mshindi kwa kutwaa mataji  mengi ya kifahari ,taifa hilo  lilitawazwa  kama  Africa’s leading destination ,huku bodi ya  utalii  Tanzania  ikipokea  heshima ya bodi ya utalii inayoongoza Afrika .

Miongoni mwa hazina za asili za Tanzania  hifadhi  ya taifa  ya Serengeti  ilipewa jina la  hifadhi ya kitaifa inayoongoza  Afrika na  mlima Kilimanjaro  ulipata tuzo  ya kivutio  kinachoongoza kwa watalii Afrika  na hivyo  kuimarisha  sifa ya Tanzania kama kivutio cha lazima cha kutembelewa na wapenda  matukio (adventure)   na wapenzi  wa asili sawa.

Sherehe za  tuzo za dunia za tuzo za Afrika za 2024 zilikuwa sherehe  bora za utalii barani Afrika  huku washindi kutoka kanda zote wakionyesha ubora Zaidi  ambao  bara  linapaswa kutoa huku  viongozi  wakiendelea kuvuka mipaka ya ukarimu na usafiri  ,hadhi ya Afrika kama kivutio kikuu cha utalii inatarajiwa kufikia kilele kikubwa Zaidi .



Comments

Popular posts from this blog

Kwale Doctors Strike Enters Day 3 Amid Chaos, Unpaid Salaries, and Deteriorating Healthcare Services

Lack of focus on sanitation and hygiene interventions puts children at risk of death due to bacterial infections causing diarrhea in Kilifi County.

CHAMA CHA UZALENDO CHA TISHIA KUJIONDOA KATIKA MUUNGANO WA AZIMIO