HAJA YA KUKOMESHA UKATILI WA KIJINSIA KENYA.

 

Wanahabari ,maafisa wa usalama,  baraza la vyombo vya habari nchini Kenya  na maafisa wa International Justice Mission.

Taarifa yake : Caroline Katana. 

Dhulma za kijinsia   ni  janga  linaloendelea kuwakumba  akinamama na watoto  si tu katika mataifa ya ukanda wa afrika mashariki  bali katika mataifa mbalimbali ulimwenguni .

Kumekuwa na kupanda  na kushuka  kwa twakimu za visa hivyo ,mataifa  yaliyo na uchumi wa wastani na yale ya uchumi wa chini yakionekana kuathirika hata Zaidi na visa hivyo .

Baadhi ya  wanaharakati  wakisema kuwa swala  la uzembe katika asasi za kushughulikia kesi hizo kuwa changizo kuu za kupanda kwa visa hivyo hususan kwa watoto huku wakitoa wito wa kimataifa kwa  wazazi  kuongeza ulinzi na ufuatiliaji wa watoto wao.

Watoto wametajwa kupitia visa vya ulawiti , ndoa na mimba za utotoni, ajira za utotoni, ulanguzi wa watoto  ,ubakaji na unajisi mikononi mwa watu wao wa karibu.

Ukatili dhidi ya watoto  bado unafichwa na kukubalika  katika baadhi ya wanajamii barani afrika, hali ambayo ina athari  kubwa  na za muda mrefu kwa maisha  ya watoto zikiwemo  za kimwili ,kiakili  na kihisia ,athari hizo  zikigusa  maendeleo yao  na elimu.

Ukatili wa kimapenzi  ukihusishwa  na unyanyapaa na machungu  ya moyoni  na unasababisha  mamba  zisizotakikana ,magonjwa  ya zinaa  na hatari  kubwa  ya kuambukizwa virusi vya HIV  kwa wavulana na wasichana.

Ingawa vitendo hivyo  ni ukiukaji  mkubwa wa haki za watoto, ubakaji, ulawiti na ukatili  bado ni vigumu kuvifanyia  utafiti kutokana na unyeti wake, takwimu  zilizoko ni hafifu na hazitoshelezi  huku  tafiti za kitaifa  zikiwa chache  na kutoa  taarifa ya vitendo  hivyo ni vigumu.

Kenya  ni miongoni mwa mataifa yaliyopitisha sheria  za nchi na zile za kimataifa  za kupambana  na dhulma za kijinsia ili kutoa ulinzi wa haki za raia wake.

Mwaka 2010 kenya iliingia katika  itifaki  ya mkataba wa afrika juu ya haki za binadamu na wanawake  wa  afrika   ( Maputo protocol ) madhumuni ikiwa ni kukuza  matumizi  ya itifaki  hii na kuchangia katika stakabadhi zinazoendeleza haki  za wanawake katika  nchi za afrika mashariki.

Kulingana  na Data  kutoka  kwa  KNBS 2022 asilimia 34 ya wanawake nchini kenya wamepitia dhulma za kijinsia  za kupigwa   wakiwa na miaka 15  na aslimia 13 wamepitia dhulma za kingono katika maisha yao.

Kaunti ya Kwale ikiwa miongoni mwa kaunti za humu nchini zinazoongoza kwa visa vya dhuma za kijinsia kama zile za  ngono jamii, ukeketaji, ulawiti, ubakaji, unajisi, mimba na ndoa za utotoni zikikithiri.

Utafiti  uliofanywa  na KDHS  2022 unaonyesha asilimia 14.8% ya wasichana wenye umri wa miaka 15-19  kaunti  ya Kwale  wamewahi kupata mimba idadi iliyotajwa kuwa ya juu.


Shirika la kimataifa  la kutetea  haki  msingi za akinama na watoto la International  Justice Mission IJM  nchini kenya  linafanya kazi pamoja na serikali ili kuimarisha mifumo ya haki za umma ili kuwalinda watu walio katika umaskini kutokana na unyanyasaji kwa kuwaokoa wahasiriwa, kuwafikisha wahalifu mbele ya sheria, na kuwasaidia walionusurika kuelekea usalama na uwezeshaji endelevu.

Mkurugenzi wa shirika la kimataifa la IJM nchini Kenya  Vincent Chahale.

 Mkurugenzi wa shirika la IJM kenya Vincent chahale  akisema kuwa   Kenya ina kiwango kikubwa cha unyanyasaji wa kijinsia ambapo 15.6% ya wasichana na 6.4% ya wavulana wamepitia ukatili wa kijinsia wakati wa utoto wao, wakati 13% ya wanawake wamepitia ukatili wa kijinsia.

Aidha bw.Chahale  amedokeza kuwa  tangu 2016, IJM imefanya kazi kwa karibu na vyombo vya habari na wadau wa serikali ili kukuza masuala na hadithi kuhusu mfumo wa haki.

“Hii inawiana vyema na maono yetu ya kulinda wanawake  milioni 18 na watoto dhidi ya ukatili nchini Kenya, na ni sehemu ya  malengo  yetu kukomesha  ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto, ambao unaendelea  Uganda na unatarajiwa kupanuka hadi Malawi, na Zambia,” Asema bw.Chahale.

Kadhalka  ameeleza  kuwa  kuenea kwa Ukatili wa Kijinsia dhidi ya Wanawake na Watoto, mapungufu katika mfumo wa haki yanamaanisha kwamba wakosaji wanatenda bila kuadhibiwa, waathiriwa hawana haki ya kupata haki au huduma za usaidizi na mamilioni ya wanawake na watoto wanaoishi katika mazingira magumu wanaishi bila ulinzi dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia.

 Tunatumai kuona mabadiliko katika  vipengele  vya kuthibiti   kuenea kwa Unyanyasaji wa Kijinsia dhidi ya Wanawake na Watoto, utendaji wa watendaji wa Mfumo wa Haki ya Jinai, imani na utegemezi wa watu katika mfumo wa haki ya jinai.

IJM inafanya kazi kwa ushirikiano huo na mamlaka za mitaa katika nchi 14. Tangu 2001, IJM imefanya kazi nchini Kenya katika mpango unaoendelea wa mageuzi ya sheria  na katika miradi mbalimbali inayolenga kuzuia unyanyasaji wa kingono kwa watoto.

Afisa wa watoto eneo bunge la Msambweni kaunti ya Kwale  Kivuli Johnstone ameafiki kuwepo na visa vya dhulma za kijinsia dhidi ya watoto eneo la Msambweni vinavyohusishwa na watu wao wa karibu.

“ Tunasikitika kwa sababu visa hivi ni vya kijamii , baadhi ya wazazi wakiume wanaoachiwa watoto  baada ya bibi zao kusafiri  Ughaibuni  kutafuta ajira  badae  wazazi hawa wakiume huwageukia watoto wao na kuwadhulumu ,”Asema bw.Kivuli.

Bw. Kivuli akielezea kuwepo na changamoto  ya watoto kwa watoto kudhulumiana kingono na watu wazima kudhulumu watoto wadogo.

Aidha  Kivuli amesema kuwa ni sharti kuwepo na mikakati ya kisheria  ya kuwalinda watoto wakati wazazi wao wakike wanaposafiri nchi za nje kutafuta ajira   ili kuhakikisha watoto hao wanabaki salama.

Hata hivyo amedokeza kuwa  wanashirikiana  na maafisa wa  wakujitolea  wa kutetea haki za watoto  nyanjani kuihamasisha jamii  kuhusiana  na athari za ukatili dhidi ya watoto.

Kisa cha hivi punde kikiwa cha mwanafunzi mmoja mwenye umri wa miaka 17 aliye katika Grade ya 8 katika shule moja huko Kinango kaunti ya Kwale aliye nyanyaswa kingono na kupewa ujauzito na mchungaji wa kanisa moja katika kijiji cha Mtobora  wadi ya Ndavaya.

Mwalimu wa shule hio akiafiki kesi hio kurekodiwa katika kituo cha polisi cha Ndavaya  na  mshukiwa   kukamatwa na kufikishwa mahakamani japo kudaiwa kuachailiwa kwa dhamana hatua ambayo anasema kuwa huenda likamnyima haki mwathiriwa.




Afisa wa maswala ya kjinsia  nchini tawi la Kwale Nelly Amoite  ameafiki  ongezeko la visa vya dhulma za kijinsia baada ya wakaazi kupata ufahamu wa kuripoti kesi hizo kinyume na ilivyokuwa hapo awali.

“ visa vya kijinsia  vimepungua kwa kiasi Fulani , japo tuko na  safari ndefu ya kupambana na visa hivyo ,tumekuwa tukiihamasisha jamii kuhusiana na athari za  dhulma za kijinsia  tuko na nambari yetu maalum  1195 ya kuripoti kesi hizo kwa wepesi na huduma hio haina malipo ,” Asema  bi Amoite.

Bi .Amoite  akikisitiza umuhimu wa usawa  wa kijinsia ili kukomesha ukatili dhidi ya wanawake na wasichana wadogo ,akisema kuwa afisi yake kwa ushirikiano na wadau mbalimbali  wanaendeleza mchakato wa kuwawezesha wanawake katika jamii.

 Idara  ya upelelezi  wa jinai DCI  imekuwa  ikisaidia sana katika kuimarisha uwezo wa serikali ya Kenya kugundua, kuchunguza, na kushtaki kesi za unyanyasaji zinazowapata wanawake na watoto kupitia programu za sekta ya haki. 

Mkurugenzi wa DCI nchini  Mohamed I.Amin  akisema kuwa shirika hilo  limekuwa mshirika mkubwa katika kufadhili programu za kuwajengea uwezo wahusika mbalimbali katika sekta ya haki, zinazolenga kuongeza ujuzi na ustadi wa kupambana na kesi hizo.

“Kama tunavyojua, ukatili dhidi ya wanawake na watoto ni suala zito ambalo linasumbua jamii yetu na  ni ukiukwaji wa haki zao msingi za binadamu na kwenda kinyume na misingi ya usawa na haki  hivyo  ni muhimu katika kufanya asasi zetu za sekta ya haki ziwe na ufanisi na  utaalumu ambao Wakenya wanaweza kuamini katika uwajibikaji  wao , Asema bw. Amini. 


Aidha  mkurugenzi  huyo  akiutaja  Ukatili dhidi ya Watoto  kuwa  tatizo la kimataifa ambalo lina matokeo mabaya sio tu kwa watoto walionyanyaswa bali pia kwa jamii kwa ujumla.

 “ Kukomesha aina zote za unyanyasaji katika familia, shuleni, na katika jamii ni jambo la muhimu sana kwa haki na ustawi wa watoto, na mustakabali endelevu , Kwa kutambua Ibara ya 53(1), ya Katiba ya Kenya inayotambua haki ya watoto wote kulindwa dhidi ya unyanyasaji, kutelekezwa, mila na desturi zenye madhara,” Ahoji bw. Amini.

Kadhalka  bw.Amin   akiafiki  vyombo vya habari  kuwa washirika muhimu linapokuja suala la kuongeza ufahamu wa kuenea kwa unyanyasaji dhidi ya wanawake na watoto, pamoja na kutambuliwa kwake kwa umma.

“ Licha ya jukumu hili muhimu katika kuongeza ufahamu na kuripoti juu ya tishio hili, kumekuwa na matukio machache ambayo yanaelekeza kwenye mtazamo wa hisia na dhana potofu katika kuripoti kwa vyombo vya habari, mara nyingi kuhusu kesi maalum, wakati idadi ya kuzuia  au elimu , ripoti za vyombo vya habari bado hazitoshi,” Asema bw. Amini.


Hata hivyo mkurugenzi huyo  amedokeza kuwa idara ya polisi nchini  NPS inalenga kushughulikia   tatizo sugu la Unyanyasaji wa Kijinsia na Jinsia (SGBV) kwa ukamilifu na kwa haraka Zaidi.

 “ NPS kwa sasa iko katika mchakato wa kutekeleza Kituo cha Majibu cha  dhulma  za kijinsia  Almaarufu  "One-Stop" kilichofahamika kama   POLICARE ("Police Cares") ,kituo hicho  kinalenga kusawazisha na kukamilisha miundo na programu zilizopo za idara ya polisi  kwa kupitisha Mtazamo wa Kisekta mbalimbali  katika usimamizi wa  dhulma za kijinsia nchini ,” Asema bw. Amini. 


Lengo kuu la kituo cha  POLICARE ni kutoa mfumo mpya  wa kusaidia na kuimarisha uwezo wa idara ya polisi  ili kufanikisha  na  kutoa majibu ya haraka kwa tatizo la  SGBV.

Sera hii inazingatia maeneo makuu matano yafuatayo , kutoa huduma kamilifu katika Kituo cha Njia Moja , kuimarisha ushirikiano  ndani ya Mfumo wa Haki ya Jinai,  kuondoa unyanyasaji na kuingiliwa kwa wahasiriwa na mashahidi,  kuwezesha haki ya haraka na kufungwa kwa kesi za unyanyasaji wa kijinsia na kuhakikisha usimamizi wa maarifa na kujenga uwezo kwa ajili ya usaidizi wa mwathirika unaofaa na haki.

Inatarajiwa kuwa mchakato  huo  utajumuisha   wadau mbalimbali, vikiwemo vyombo vya habari, ili kuleta mafanikio katika maeneo yote yaliyolengwa.

Hakimu mkaazi na msimamizi wa mahakama ya Kwale Lilian Lewa akisema kuwa kulingana na sheria  ya kulinda haki za watoto  Sexual Offences Act  mtu yeyote atakayepatikana na kosa la kumnajisi mtoto chini ya umri wa miaka 9 anahukumiwa kifungo cha maisha  na atakayepatika na hatia ya kubaka mtoto 13 hadi 15 anahukumiwa miaka 20 gerezani na atakayepatikana akibaka mtoto wa miaka 15 hadi 18 anahukumiwa miaka 15 gerezani.




 









Comments

Popular posts from this blog

Kwale Doctors Strike Enters Day 3 Amid Chaos, Unpaid Salaries, and Deteriorating Healthcare Services

Lack of focus on sanitation and hygiene interventions puts children at risk of death due to bacterial infections causing diarrhea in Kilifi County.

CHAMA CHA UZALENDO CHA TISHIA KUJIONDOA KATIKA MUUNGANO WA AZIMIO