IDADI YA REFARII /WAAMUZI WAKIKE WANAOFUZU KILA MWAKA YAONGEZEKA KWALE.

Waamuzi wakike katikati ya uwanja na pembeni.

Taarifa yake : Caroline Katana 

Katika soka  refarii anakuwa na nafasi kubwa sana ya kuufanya mchezo  wa soka kuwa mzuri au kuuharibu.

Katika  soka refarii anakuwa na kazi ya kusimamia sheria za mchezo  wa soka na kama  muamuzi wa mwisho  katika mechi , refarii  ndio  ana uwezo  wa kuamuru pambano liendelee au lisiendelee.

Jumapili  iliyopita  waamuzi wa kike wanane kati ya waamuzi 26 walifuzu  kuchezesha timu  mbalimbali za soka kaunti ya Kwale na hata  ligi za  taifa.

Mafunzo hayo yalitolewa na shirika la Sambasports Youth Agenda  kwa ushirikiano na usimamizi wa kampuni ya uchimbaji madini  ya Basetitanium  na shirikisho la soka la FKF tawi la Kwale.

Idadi ya  waamuzi wa kike inaongezeka  pia ,mwaka wa  2013 refarii  wakike  watano  walifuzu kati  ya refarii ishirini na nne  waliopokea mafunzo hayo.

Ubaguzi  wa kijinsia kutoka kwa wachezaji  na watazamaji ,ukosefu  wa kuajiriwa kwa wanawake katika fani hio  na  vyombo vya soka ,dhana hasi  za watazamaji  ni baadhi ya vikwazo  vinavyowakabili wanawake katika kusimamia  mechi za soka na michezo mingine kwani hutunga mazingira ya uhasama  kwa taaluma hii.

Refarii Abigael Ndizi
Abigael Ndizi ni mmoja wa waamuzi wakike waliofuvu siku ya Jumapili , akisema kuwa  hatua hio ni fursa ya kufungua mlango  na kuonyesha kwamba wanawake wote  wana uwezo  wa  kusimamia michezo kama wanaume.

“Tumekuwa tukijifunza kwa bidii  sana  kwa sababu  wengine husema  wanawake  hawawezi kukimbia kwa kasi ya wanaume  ndio maana hatuwezi kuwa wanaume ,lakini  tunaweza kufanya tuwezavyo kuwa katika kiwango sawa ,” Asema bi Ndizi.

Bi .Ndizi   akisema kuwa ndoto yake ni  kujiunga na waamuzi  wakike duniani na kuchezesha mechi za kimataifa ,akiitaja hatua hio kuondoa dhana potofu dhidi ya mtoto wakike katika Nyanja ya soka.

“ Hakuna kitu ambacho hakiwezekani ,niling’ang’ana sana kati ya wanaume saba na nikaibuka kuwa muamuzi wa katikati  ,akinadada wasiogope kujiunga katika Nyanja hii ya soka  wajitokeze na wakuze talanta zao ,” Asema bi .Ndizi.

Refarii Omar Abdallah Kimwaga

Omar Abdallah kimwaga mwakilishi wa London FC  aliyeshiriki katika mafunzo hayo ya  refarii ametaja mafunzo hayo kumuwezesha kuzifahamu sheria kumi na saba za soka .

“Mimi kama refarii wa katikati  nimezielewa Zaidi sheria za mchezo wa soka  na nina uwezo wakuwafunza  hata mashabiki  walio na tabia za kuwakosoa  refarii kwa kukosa kuzifahamu sheria  ,”Asema bw Kimwaga.


Hata hivyo refarii Kimwaga amedokeza kuwa yuko tayari kukabiliana na changamoto za aina yeyote katika mchezo huo wa soka.

mwenyekiti wa shirikisho la FKF Kwale Hamisi Mwakoja

Mwenyekiti wa shirikisho la FKF kaunti ya Kwale Hamisi Mwakoja amehoji kuwa katika soka ya kiulimwengu malengo  ya FIFA  ni kuona kuwa kuna timu za akinadada na zile za wanaume  zinacheza  ligi sawa  kufikia mwaka 2032.

Hata hivyo ameafiki kuwa   dhana potofu za mashambulizi mabaya ya refarii na masaa ya  kucheza  soka  kuwa kikwazo cha akinadada wengi  kujiunga na fani  ya urefarii .

“Kuna hofu kuwa mwanadada akiwa refarii anaweza kushambuliwa wakati wowote ,na hii imekuwa changamoto kwetu sisi kuwapata akinadada wengi ,”Asema bw.Mwakoja .

Kadhalka amehoji kuwa kaunti ya Kwale hadi sasa iko na  refarii 268 miongoni mwao wakiwa akinadada.

Kiongozi huyo wa FKF   akilitaja shirika la Sambasports Youth Agenda na usimamizi wa kampuni ya base titanium kuchangia pakubwa ukuaji wa soka katika kaunti ya Kwale.

Mkurugenzi wa sambasports youth agenda Mohamed Mwachausa

Mkurugenzi wa shirika la Sambasports Youth Agenda  Mohamed Mwachausa  akisema kwamba malengo makuu  ya shirika hilo  ni kukuza talanta na kudhibiti tabia potofu miongoni mwa vijana kupitia mafunzo ya urefarii na makocha.


“ Hii ni awamu ya pili ya kufundisha   refarii kaunti ya  Kwale kupitia ushirikiano wa FKF  na ufadhili wa basetitanium  ,mwaka jana mwezi wa kumi  tulifundisha  refarii  ishirini na wane na watano walikuwa akinadada ,tulipanga kuwafundisha akinadada Zaidi ya kumi  lakini haikuwa rahisi kuwapata ,mwaka huu imekuwa rahisi kuwapata kwa sababu walipata motisha ya wale refarii wakike tuliowafundisha mwaka jana kutokana na sifa za kazi nzuri wanayofanya uwanjani pamoja  weledi wao katika fani hio  ,tuna Imani mwakani tunaweza kupata wasichana Zaidi  katika fani hii ya urefarii na ukufunzi ,”Asema bw.Mohamed.

 Bw.Mwachausa kadhalka amewata  refarii hao na wachezaji kwa ujumla kudumisha nidhamu ,akisema kuwa talanta bila nidhamu hulipa hasara badala ya faida.

Bw.Mwachausa aliyekuwa akizungumza katika kipute cha fainali ya  Bongwe  soka For Peace kati ya Bongwe United na Diani Stars  ameelezea kuimarika kwa usalama katika eneo hilo  baada ya kushuhudiwa kwa visa vya utovu wa usalama  miezi michache iliyopita.

“ Sababu iliyotuleta  hapa ilikuwa ni utovu wa nidhamu miongoni mwa vijana  na taasubi kuwa eneo hili halina amani  na usalama ,tumekuja kwa miezi mitatu na hatujashuhudia  purukushani ya aina yeyote na ndio maana leo hii tunasherehekea ujio wa amani na usalama katika lokesheni hii  ya Diani,” Asema bw.Mohamed.

mwakilishi wa wanawake Kwale Fatuma Masito 

Mwakilishi wa wanawake kaunti ya  Kwale Fatuma Masito  ameahidi kushirikiana na shirika la Sambasports Youth Agenda na shirikisho la FKF  Kwale katika mchakato huo wakukuza talanta za vijana ili kuhakikisha kwamba wanajinasua katika jinamizi la utumizi wa mihadarati na visa vya   utovu wa usalama.

Aidha ameelezea kuridhishwa kwake na jinsi akinadada walivyojitosa katika fani ya soko ,akiitaja kama njiamojawapo ya kuepuka dhulma za kijinsia katika jamii .

 Ngarambe hio ya fainali  ya siku ya jumapili katika uwanja wa Shamu , timu ya Bongwe United  iliibuka  na ushindi wa bao  mbili  dhidi ya Diani Stars waliopata bao moja.




Comments

Popular posts from this blog

Kwale Doctors Strike Enters Day 3 Amid Chaos, Unpaid Salaries, and Deteriorating Healthcare Services

Lack of focus on sanitation and hygiene interventions puts children at risk of death due to bacterial infections causing diarrhea in Kilifi County.

CHAMA CHA UZALENDO CHA TISHIA KUJIONDOA KATIKA MUUNGANO WA AZIMIO