SEKTA YA UVUVI KWALE YAPIGWA JEKI
Taarifa yake : Caroline Katana
Sekta ya uvuvi kaunti ya Kwale inatarajiwa kuimarika hata zaidi baada ya makundi ya wasimamizi wa bahari ( Beach Management Units ) kupokea boti nane za kisasa chini ya ufadhili wa Jumuiya ya Ulaya EU kupitia mradi wa Go- Blue na serikali ya kaunti kupitia mradi wa KEMFSED .
Boti tano zilizofadhiliwa na EU zitawafaidi wavuvi kutoka eneo la Shimoni , Kibuyuni na Mkwiro huko boti tatu za ulinzi ( patrol boats ) zilizofadhiliwa na serikali ya Kwale kupitia mradi wa KEMFSED zitatumika na wavuvi katika sehemu za ushirika za Shimoni –Vanga, Mwandamu- Funzi na Chale- Gazi.
Zaidi ya wakaazi elfu kumi kusini mwa pwani wanategemea bahari moja kwa moja kujikimu kimaisha .
Nchini kenya ,uvuvi unajumuisha Zaidi maji chumvi ( maziwa ,mito na mabwawa ) ,pwani na baharini ( bahari hindi) na ufugaji wa samaki .
Uzalishaji wa samaki kwa mwaka unakadiriwa kuwa tani 150,000 huku sekta hio ya uvuvi kwa sasa inachangia takribani asilimia 0.5 kwenye pato la taifa ( GDP)
Akizungumza huko Shimoni wakati wa kukabidhi boti hizo kwa wavuvi ,naibu gavana wa Kwale Chirema Kombo ameipongeza Jumuiya ya Ulaya kwa kupiga jeki sekta hio ya uvuvi.
“Mpango huu utahakikisha uvuvi salama na kuchangia kuimarika kwa kiwango cha mapato kwa wavuvi na kuboresha hali zao za maisha kinyume na ilivyokuwa hapo awali ambapo walitumia vifaa duni vya uvuvi hali iliyowapelekea kupata mapato duni ,”Asema bw.Chirema.
Aidha kiongozi huyo amewataka wavuvi waliopokea boti hizo kuzitunza ili kuhakikisha zinawafaidi kikamilifu ili kuafikia ndoto zao za ufanisi kupitia sekta hio .
“ Boti hizi mkizitunza ni kwa manufaa yenu ,sisi kama serikali ya kaunti tunashirikiana na washikadau mbalimbali ili kuhakikisha maisha ya wakaazi yanaboreka kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo huu ukiwa miongoni mwao ,”Ahoji bw.Chirema.
Kwa upande wake meneja wa mradi wa Go –Blue Lorenzo Colonna Preti amesema kwamba Jumuiya ya Ulaya EU itaendelea kupiga jeki shughuli za maendeleo kaunti ya Kwale na ukanda mzima wa pwani ili kubadilisha hali za maisha za wakaazi .
Bw.Preti akisisitiza umuhimu wa wavuvi kutumia boti za kisasa katika shughuli zao kama njiamowapo ya kukomesha uvuvi haramu .
Mwenyekiti wa makundi ya usimamizi wa bahari BMUs kaunti ya Kwale ambae pia ni mwenyekiti wa Mkwiro BMU Mtengo Omar Makame ameafiki awali kuwepo na uvuvi haramu kutokana na utumizi wa vifaa duni vya uvuvi hivyo kusema kuwa boti hizo zitakuwa suhulu la kudumu la changamoto hio.
“ Ufadhili huu kwetu tumeupokea vyema kwani utaboresha sekta yetu ya uvuvi tuliyoitegemea kama mtaji wetu na pia boti zile za ulinzi zitahakikisha wavuvi wanaendeleza shuguli zao katika mazingira salama ,”Asema bw.Mtengo
Waziri wa kilimo ,uvuvi na ufugaji kaunti ya Kwale Roman Shera amedokeza kuwa boti hizo zina uwezo wa kufika katika maji ya wastani japo kusema kuwa serikali yak wale kupitia mradi wa KEMFSED inanua kuwanunulia wavuvi boti kubwa zenye uwezo wa kufika katika maji ya kina kirefu katika bahari hindi ili waweze kupata samaki wa kutosha watakao wawezesha kupata kipato bora Zaidi.
Aidha amedokeza kuwa serikali ya kaunti ya Kwale kwa ushirikiano na walinzi wa bahari ( coast guard ) na shirika la uhifadhi wa wanyamapori KWS wanaendeleza mchakato wa kuwahamasisha wavuvi kuhusiana na sheria hitajika za uvuvi ili kukomesha uhasama kati yao na maafisa wa coast guard unaotokana na uvunjwaji wa sheria za bahari na wavuvi hao wanapoendeleza shughuli zao



Comments
Post a Comment