JESHI LA KENYA KUPANDA MITI KATIKA JUHUDI ZA KUREKEBISHA SEHEMU ZILIZOCHIMBWA MADINI NA KAMPUNI YA BASETITANIUM

wanajeshi wa majini[kenya navy] wakipanda miti base titunium kwale.

Taarifa  yake : Caroline Katana 

Usimamizi wa kampuni ya uchimbaji madini ya basetitanium umetia kasi zaidi katika zoezi la upanzi wa miti ili kuzirekebisha sehemu zilizochimbwa madini na hakuhakikisha mazingira  bora na salama  wakati watakapofungasha virago vyao mwishoni mwa mwaka huu.

Kampuni hiyo imekuwa ikichimba madini  ya  thamani  tangu mwaka 2013, na kuchukua takriban  asilimia 65  ya sekta ya madini nchini kufuatia mapato ya juu ya madini.

Aidha usimamizi wa kampuni hio  sasa unaendelea na upanzi wa miti na nyasi katika sehemu zilizochimbwa madini  ili kuzifanya sehemu hizo  ziwe na manufaa  kwa uzalishaji  chakula  baada ya shughuli za uchimbaji kukamilika.

Meneja mkuu wa masuala ya nje katika kampuni hio  ya basetitanium Simon Wall anasema ukarabati  na uhifadhi wa ardhi  umekuwa sehemu muhimu ya mzunguko  wa maisha  ya uchimbaji  madini kwani  umewezesha matumizi  salama  na yenye tija ya baadaye.

Meneja mkuu, masuala ya nje katika kampuni ya basetitanium Simon Wall.

 ” Shughuli za urekebishaji  katika maeneo yaliyochimbwa  zitahakikisha  ardhi  ni salama ,tulivu na inarudi katika hali  endelevu na inayoweza kutumika ,”Asema bw.Wall.

Wall alikuwa akizungumza na wanahabari katika zoezi la upanzi wa miti lililoongozwa na wanajeshi kutoka jeshi la wanamaji  la Kenya  katika  eneo la South dune  katika eneo la mgodi  kaunti ya Kwale.

  Bw .Wall amesema  usimamizi wa basetitanium unatambua  jeshi la wanamaji  la kenya kama mshirika muhimu na aliyoonyesha  nia ya miradi ya ushirikiano  wa kimazingira  

 “ Hadi  sasa kukarabati  zaidi ya hekta 500  za ardhi  katika  milima ya kusini  na kati  ambayo imefanikiwa ,”Asema bw,Wall.

Kadhalka bw.Wall ameafiki  Zaidi ya miti  800  kutoka kwenye  kitalu cha basetitanium imepandwa  katika maeneo yaliyochimbwa  ili kuanza kuboresha  bianuwai  ya eneo hilo  na kurudisha ardhi kama  ilivyokuwa  au bora Zaidi kabla ya uchimbaji kuanza mwaka 2013.

Kwa upande wake  kanali Benson  Kariumbo ,mkuu wa chuo cha  mafunzo  ya wanamaji  cha  Kenya Navy Training  College , Mombasa  amesema kuwa  zoezi la upandaji miti  katika maeneo  yaliyochimbwa  madini  ilikuwa sehemu  ya kampeni  ya upandaji  miti iliyozinduliwa kwa ajili ya maandalizi  ya sherehe  za kuadhimisha miaka 60  ya jeshi la wanamaji  la Kenya  mwezi Disemba 2024.

Kanali Kariumbo akisema juhudi  za upandaji miti ni chini ya ufadhili  wa mpango wa mazingira  wa  jeshi la ulinzi la  kenya ,akibainisha kuwa kukabiliana na mabadiliko  ya hali ya hewa ni juhudi za pamoja.

kanali Benson  Kariumbo ,mkuu wa chuo cha  mafunzo  ya wanamaji  cha  Kenya Navy Training  College , Mombasa.

“ Huu ni mpango ambao tumekuwa tukiutekeleza kama wanajeshi  katika miaka ya hapo awali kupitia program yetu maalum inayofahamika  kama environmental  soldier program ,hii tuliianzisha baada ya kuhimizwa kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira ,” Asema  kanali Kariumbo. 

Kanali huyo akisema  siku ya  wanamaji wa Kenya huadhimishwa kila mwaka mnamo tarehe 14 Disemba  kuadhimisha kuanzishwa kwa jeshi la wanamaji la Kenya na  kuheshimu mafanikio yake  kwa miaka mingi.

“Tunafurahi kushiriki  katika juhudi  za kuongeza uwezo wa kushughulikia  masuala ya mazingira  yanayohusiana  na sekta ya madini ,”Asema kanali Kariumbo.

Aidha amesema kuwa mpango huo wa  kulinda mazingira ni sehemu ya mpango wa kitaifa wa upandaji miti unaolenga kuinua  miti nchini hadi asilimia 30 kama juhudi za kujikimu na kukabiliana na mabadiliko tabia nchi.



Comments

Popular posts from this blog

Kwale Doctors Strike Enters Day 3 Amid Chaos, Unpaid Salaries, and Deteriorating Healthcare Services

Lack of focus on sanitation and hygiene interventions puts children at risk of death due to bacterial infections causing diarrhea in Kilifi County.

CHAMA CHA UZALENDO CHA TISHIA KUJIONDOA KATIKA MUUNGANO WA AZIMIO