MAPANGO YA AMBONI TANGA TANZANI URITHI WA ASILI AFRICA
Leo, tunakuletea moja
ya maajabu ya kiasili yaliyopo Tanga, Tanzania — Mapango ya Amboni.
Mapango haya ya kale
yanatajwa kuwa miongoni mwa mapango makubwa ya mawe ya chokaa (limestone)
katika Afrika Mashariki.”
wa zaidi ya miaka
milioni 150, yakitokana na mabadiliko ya miamba katika enzi za Jurassic.
Mwaka 1892, kampuni ya
Amboni Ltd ilikuwa ya kwanza kuyamiliki kabla ya serikali ya kikoloni kutangaza
eneo hili kuwa la kihifadhi mwaka 1922.
Hadi leo, mapango haya
yanasimamiwa na Idara ya Urithi wa Taifa NCHINI TANZANIA.”
“Katika mapango haya
zaidi ya kumi, ni moja tu ndilo linalotembelewa na wageni huku sababu hal;isi
iukiwa bado kuwekwa bayana.
Ukitembea ndani,
utakutana na mawe yenye maumbo ya kipekee – kama vile kiti cha enzi, mfuko wa
sofa, meli, hadi sanamu inayofanana na Statue of Liberty!
Hii ni ishara ya
maumbile kuchonga sanaa yake yenyewe kwa muda mrefu.”
“Mapango haya si tu
kivutio cha watalii, bali pia ni sehemu takatifu kwa jamii za Segeju, Digo,
Sambaa na Bondei.
Katika baadhi ya
sehemu za ndani, unakuta madhabahu ya kutoa sadaka na kuomba baraka kutoka kwa
mizimu.
Hadithi nyingi za kale
kuhusu watu waliopotea au kupokea ishara za kiroho huimarisha imani kuwa haya
si mapango ya kawaida.”
Comments
Post a Comment