MAPANGO YA AMBONI TANGA TANZANI URITHI WA ASILI AFRICA




Leo, tunakuletea moja ya maajabu ya kiasili yaliyopo Tanga, Tanzania — Mapango ya Amboni.

 

Mapango haya ya kale yanatajwa kuwa miongoni mwa mapango makubwa ya mawe ya chokaa (limestone) katika Afrika Mashariki.”

 

wa zaidi ya miaka milioni 150, yakitokana na mabadiliko ya miamba katika enzi za Jurassic.

 

Mwaka 1892, kampuni ya Amboni Ltd ilikuwa ya kwanza kuyamiliki kabla ya serikali ya kikoloni kutangaza eneo hili kuwa la kihifadhi mwaka 1922.

 

Hadi leo, mapango haya yanasimamiwa na Idara ya Urithi wa Taifa NCHINI TANZANIA.”

“Katika mapango haya zaidi ya kumi, ni moja tu ndilo linalotembelewa na wageni huku sababu hal;isi iukiwa bado kuwekwa bayana.

Ukitembea ndani, utakutana na mawe yenye maumbo ya kipekee – kama vile kiti cha enzi, mfuko wa sofa, meli, hadi sanamu inayofanana na Statue of Liberty!

 

Hii ni ishara ya maumbile kuchonga sanaa yake yenyewe kwa muda mrefu.”

“Mapango haya si tu kivutio cha watalii, bali pia ni sehemu takatifu kwa jamii za Segeju, Digo, Sambaa na Bondei.

 

Katika baadhi ya sehemu za ndani, unakuta madhabahu ya kutoa sadaka na kuomba baraka kutoka kwa mizimu.

 

Hadithi nyingi za kale kuhusu watu waliopotea au kupokea ishara za kiroho huimarisha imani kuwa haya si mapango ya kawaida.”


Comments

Popular posts from this blog

Kwale Doctors Strike Enters Day 3 Amid Chaos, Unpaid Salaries, and Deteriorating Healthcare Services

Lack of focus on sanitation and hygiene interventions puts children at risk of death due to bacterial infections causing diarrhea in Kilifi County.

CHAMA CHA UZALENDO CHA TISHIA KUJIONDOA KATIKA MUUNGANO WA AZIMIO