UKATILI WA WAZAZI KWALE
Johnstone Kivuli afisa wa maswala ya watoto Msambweni. Taarifa yake : Caroline Katana Wizara ya watoto kaunti ya Kwale imekemea vikali vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto na baba zao wakati wazazi wao wakike wanaposafiri mataifa ya nje kutafuta ajira. Hii ni baada ya afisi hio kuanza kurekodi idadi ya juu ya kesi hizo za watoto waliochiwa wazazi wa kiume kupitia dhulma za kingono. Afisa wa watoto eneo bunge la Msambweni Jonstone Kivuli akielezea kusitikishwa kwake na jinsi watoto wachanga wanavyodhulumiwa haki zao na watu wanaofaa kulinda haki zao. “ Kwa sasa hivi nashughulikia kesi mbili mahakamani za watoto waliodhulumiwa kingono na baba zao ,hizi ni kesi ambazo awali hazikuwa zinasikika lakini kwa sasa hivi tumeona hizi kesi zikiripotiwa kwa wingi katika afisi zetu ,” Asema bw.Kivuli. Utafiti uliofanywa na Kenya Demographic and Health Survey KDHS 2022 unaonyesha asilimia 14.8% ya wasichana wenye umri wa miaka 15-19 kaunti ya Kwale wamewahi kupata mimba idadi iliyotajwa ku...