Posts

Showing posts from July, 2024

HAJA YA MASHIRIKA YA KIJAMII KUSHIRIKIANA ILI KUENDELEZA MIRADI MASHINANI , ENEO LA MATUGA

Image
washirika wa mradi wa Participatory grant making Taarifa yake : Caroline Katana Mshirikishi wa mradi wa mpango wa pamoja wa kimikakati ya hatua za dini JISRA Kenya Zena Hassan , ametoa changamoto kwa makundi matano ya kijamii yaliyokuwa yakiendeleza miradi mbalimbali kwa jamii eneo la Matuga kaunti ya Kwale chini ya awamu ya pili ya mradi wa Participatory Grant Making (PGM2 ) kushirikiana kwa ukaribu na washika katika idara mbalimbali ili kuhakikisha uendelevu wa miradi hio . Hii ni baada ya mradi huo wa PGM 2 ulionza rasmi mwezi Machi mwaka huu kuingia kikomo mwishoni mwa mwezi huu wa saba kaunti ya Kwale ,awamu ya tatu ikitarajiwa kutekelezwa kaunti ya Isiolo kuanzia mwezi Agosti . Akizungumza na wanahabari baada ya kukamilika kwa mkao wa kutathmini miradi iliypkuwa ikitekelezwa na makundi hayo kilichowaleta pamoja wadau mbalimbali katika ukumbi wa mikutano wa Tiwi social hall ,bi Hassan amesisitiza umuhimu wa miradi hio kuendelezwa ili kutatua changamoto za kimsingi zinazo dumaza uk...

RAIS RUTO APONGEZWA KWALE HUKU ALI HASSAN JOHO NA SALIM MVURYA WAKITAKIWA KUEKA KANDO TOFAUTI ZA KISIASA.

Image
  wakaazi wa Kwale Taarifa yake : Caroline Katana  Wakaazi  kaunti ya Kwale sasa wanamtaka  waziri mteule Salim Mvurya na mwenzake  Ali Hassan Joho kueka  kando tofauti zao za kisiasa  na badala yake kushirikiana katika swala zima la kuhudumia taifa baada ya rais Wiliam  Ruto kuwateuwa katika wizara ya biashara  na uekezaji na ile ya madini na uchumi samawati  mtawalia . Kauli zao zinajiri baada ya rais Ruto kuvunja baraza la mawaziri  siku chache zilizopita  na kulifanyia mabadiliko ambapo  Salim Mvurya  ambae ameteuliwa kama waziri wa biashara na uekezaji aliishikilia wizara ya madini na uchumi samawati katika baraza lililopita. .Hamisi Juma Shomali Wakiongozwa na Hamisi Juma  Shomali  wameipongeza hatua ya rais Ruto kumrudisha katika wizara ,waziri Salim Mvurya ,wakiitaja hatua hio kuonyesha heshima kubwa kwa wakaazi wa Kwale na pwani nzima kwa ujumla . “Wakati baraza la mawaziri lilipovunjwa  sisi k...

CHAMA CHA UZALENDO CHA TISHIA KUJIONDOA KATIKA MUUNGANO WA AZIMIO

Image
wanachama wa CCU Taarifa yake ,Caroline Katana  Chama Cha Uzalendo  C C U  kimetishia kujiondoa katika muungano wa Azimio  na kujiunga na chama cha Wiper  ili kumpa nafasi kinara wa muungano huo Raila Odinga kujiunga na serikali ya Kenya Kwanza ili kuendeleza mazungumzo  ya kutatua changamoto msingi zinazolikumba taifa la Kenya  . Hii ni baada ya  chama  cha Uzalendo  kujitenga  na  mazungumzo  ya kitaifa  yanayopangwa na srikali  ya  Kenya  Kwanza  . Kinara wa  CCU   Richard Onsongo amesema kwamba kinara wa Azimio Raila Odinga anajipendekeza katika serikali ya Kenya Kwanza ili apate  kutengeza  nafasi za vyeo  katika serikali hio  swala ambalo hawaliungi mkono. . kinara wa chama cha ccu Kenya Richard Onsongo  Aidha amesema kwamba kuna haja ya rais Wiliam  Ruto  kubeba msalaba wake wenyewe katika maswala ya utatuzi wa changamoto zinazolikumba taifa ...

SHULE YA MSINGI YA WAA YANG’AA KIMAZINGIRA KUPITIA UFADHILI WA VYOO KUTOKA KWA KAMPUNI YA MOZZART BET KWA USHIRIKIANO NA WAKFU WA RASHID ABDALLAH .

Image
  Usimamizi wa kampuni ya Mozart bet pamoja na wadau mbalimbali. Wakfu wa  Rashid  Abdallah  umeukabidhi  rasmi  usmimamizi  wa shule ya msingi ya Waa  mradi wa vyoo  18, madawati 100, sodo miongoni mwa pembejeo zenginezo  za elimu ,  kupitia ufadhili wa kampuni ya ubashiri ya Mozatt bet  uliogharimu  takriban shilingi million 3.4. Hatua hio imejiri  kufuatia hali mbaya ya vyoo iliyokuwa ikishuhudiwa shuleni  humo iliyohofiwa kusababisha mikurupuko  ya maradhi yanayotokana na mazingira chafu. Mkurugenzi mkuu wa mozzart bet nchini Kenya  SaS'a  Krneta. Mk Mkurugenzi  wa kampuni hio ya Mozzart bet nchini kenya Sas’a Krneta amesema kwamba mazingira bora ya vyoo  utaimarisha hali ya usafi shuleni humo na kuhakikisha usalama wa kiafya kwa wanafunzi na walimu . “ Tumewakabidhi vyoo kumi na 18 ,saba  vitatumika na wanafunzi wakiume  vyengine saba  viwasaidia wanafunzi wakike huku ...

SERIKALI YA KAUNTI YA KWALE YA KOSOLEWA NA WATETEZI WA HAKI ZA KIBINADAAM

Image
  Watetezi wa haki za binadaam Kwale. Taarifa yake ,Caroline Katana Wadau mbalimbali wa kutetea haki za kibinaadam wameikosoa vikali serikali ya kaunti ya Kwale kwa kukosa kutenga fedha za kuitekeleza sheria ya jinsia 2023 katika mwaka wa kifedha wa 2024/2025 . Haya yameibuka katika mkao wa kujadili sheria hio uliowaleta pamoja wadau mbalimbali wakutetea haki za kibinadam ,idara ya watoto na maafisa wa idara mbalimbali kaunti ya kwale ulioandaliwa na shirika la Akili Dada huko Diani . Katika mkao huo ongezeko la visa vya dhulma za kijinsia limeibuka ,visa vingi vikinakiliwa katika eneo bunge la Lungalunga ambapo wasichana wenye umri mdogo wakitajwa kuwa waathiriwa wakuu ,wadi ya Dzombo ikirekodi visa 20 vya mimba za mapema mwezi Juni . Akizungumza na wanahabari pembezoni mwa mkao huo afisa wa mradi wa warsha katika shirika la Akili Dada Nancy Mutola amesema kuwa mapungu yaliyopo katika sheria hio huenda yakapelekea waathiriwa kuendelea kukosa haki endapo hayatajalizwa kwa wakati . ...

WAKAAZI ELFU 20 KAUNTI YA KWALE WAFAIDIKA NA CHAKULA CHA MSAADA KUTOKA KWA SERIKALI.

Image
Wakaazi wa Wadi ya Tsimba Golini wakipokea chakula cha ruzuku. KITAIFA Taarifa yake , Caroline Katana. Wakaazi elfu 20 kutoka familia zisizobahatika kaunti ya Kwale ni miongoni mwa wakenya wanaoelendelea kufaidika na chakula cha msaada kutoka kwa serikali ya kitaifa kupitia wizara ya mipango maalum (special programs) . Mbali na mradi wa inua jamii , wizara hio ya mipango maalum inaendeleza mradi wa utoaji chakula kwa wajane ,watoto mayatima ,wazee ,wagonjwa na watu wanaoishi katika lindi la umaskini kote nchini. Bi.Mwanaisha Chidzuga katika mahojiano  . Akizungumza wakati wa ugavi wa chakula hicho katika wadi ya Tsimba-golini huko Matuga kaunti ya Kwale naibu msemaji katika afisi ya Rais Mwanaisha Chidzuga ,amesema kwamba hatua hio ni baadhi ya mikakati ya serikali kuhakikisha wakenya wasizojiweza wanapata lishe kama wakenya wengine . “ Zaidi ya wakaazi elfu moja hapa wadi ya Tsimba-golini watapokea chakula ,na katika awamu hii ya kwanza nina lenga wakaazi elfu 20 katika kaunti ya ...

ZIARA ZA RAIS KATIKA MATAIFA YA NJE ZA CHANGIA KUKUA KWA UTALII NCHINI

Image
                           Pich: washikadau wakiokota wakataka fuo ya Diani Kwale Safari za nje za rais wa jamhuri ya kenya William Ruto zimetajwa kuwa na mchango mkubwa katika uimarishaji wa sekta ya  utalii humu nchini . Rais Ruto ametajwa kuwa mstari wa mbele kuuza utalii wa kenya katika ziara zake kote ulimwenguni. Katibu katika wizara ya utalii nchini John Ololtwaa aliyekuwa akizungumza  huko  katika fuo ya bahari ya Kongo  kaunti ya Kwale  baada ya zoezi la kusafisha fuo ya bahari ya Diani  ,amesema kuwa idadi kubwa ya watalii wanaozuru taifa hili inatokana na ushawishi wa rais Ruto  anapokuwa katika mataifa ya kigeni . “ Na rais wetu wenyewe ameweza kuinua nchi yetu na yale mambo ambayo anaongea katika mataifa ya nje na yale mambo  ambayo ana   fanya  humu nchini ,tuko na mpango wa kuinua taifa hili huko  Turkana  kupitia mpango wa Kenya is  H...