VIJANA KWALE WALAUMIWA KUPUUZA VIKAO VYA MAONI, WATAHADHARISHWA KUPITWA NA MAENDELEO
Na Mwandishi Wetu Jumwa Kwale Wito umetolewa kwa vijana katika kaunti ya Kwale kujitokeza kwa wingi kushiriki vikao vya maoni vinavyoandaliwa katika maeneo yao, huku ikielezwa kuwa wengi wao wameendelea kubaki nyuma kimaendeleo kutokana na tabia ya kutohudhuria mikutano hiyo muhimu ya kijamii na kiutawala. Imeelezwa kuwa kupitia vikao hivyo, wananchi hupata nafasi ya kutoa maoni yao kuhusu miradi na maendeleo wanayotaka kuona katika maeneo yao, lakini vijana wengi wamekuwa wakikosa kushiriki licha ya kuwa wao ndio nguvu kazi ya taifa. Changamoto hiyo imewafanya wanaharakati na mashirika ya kijamii kuanza kutafuta mbinu mpya zitakazowavutia vijana kuhudhuria vikao vya maoni kwa hiari yao bila kusubiri mialiko rasmi. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa INUA-IG katika kaunti ya Kwale, Mwenyekiti wa shirika la Tulinde Future Yetu Initiative , alisema mradi huo unalenga kuwaelimisha vijana, kina mama na watu wanaoishi na ulemavu kuhusu masuala ya utawala bora, uwajibikaj...