Posts

Showing posts from July, 2026

Serikali ya Kwale yarejesha barabara ya umma ya kuingia ufukweni Diani

Image
Na Shokah Juma Serikali ya Kaunti ya Kwale kwa ushirikiano na Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) imerejesha eneo la umma la ekari 1.14 lililotengwa kwa ajili ya barabara ya kuingia ufukweni katika eneo la Diani, Kaunti Ndogo ya Msambweni, lenye thamani ya takriban Sh45 milioni. Eneo hilo lilikuwa limenyakuliwa na kampuni binafsi kwa zaidi ya miongo mitatu, hali iliyowazuia wananchi, wavuvi na wafanyabiashara wa ufukweni kutumia njia hiyo kufikia Bahari ya Hindi. Kurejeshwa kwa ardhi hiyo kunafuatia uamuzi wa Mahakama ya Mazingira na Ardhi ya Kwale uliotolewa Julai 14, 2026, uliobatilisha mkataba wa upangishaji wa miaka 99 uliotolewa mwaka 1994 pamoja na cheti cha umiliki, na kuagiza eneo hilo lirejeshwe kuwa mali ya umma. Akizungumza wakati wa kukabidhiwa rasmi kwa eneo hilo, Gavana wa Kwale Fatuma Achani alisema hatua hiyo ni ushindi dhidi ya unyakuzi wa ardhi na itasaidia kurejesha haki kwa wananchi waliokosa fursa ya kutumia mali ya umma kwa miaka mingi....

All Eyes on Salim Kumaka as Dock Workers Union Election Race Intensifies.

Image
Former Kenya Ports Authority (KPA) Defined Contribution (DC) Scheme officer Salim Kumaka is faced with the challenge of whether to take paid leave pending retirement or contest for the Dock Workers Union (DWU) top post in union election slated for August 13. The other option left to Kumaka who is KPA operations officer is for  him to resign from the state corporation and take part in next month’s election where he enjoys government backing. He has however remained mute about his stand as to whether he will join the race to replace embattled General Secretary Simon Sang or not. The move will make the DWU election a two-horse race between him and former DWU assistant general secretary Mr Abubakar Abdillahi as they await the election board to be constituted. The purported DWU General Secretary Suliman Otieno Owuor who enjoys the support of the Central Organization of Trade Unions COTU (K) has declined to comment. The 5000 union members are already in an election mood after...

Campaigns Heat Up Ahead of August 13 Dock Workers Union Elections

Image
Former Dock Workers Union (DWU) assistant general secretary Abubakar Mohammed Abdullahi is already in a campaign trail ahead of the election. He is the only aspirant so far who has declared his interest to replace embattled Simon Sang as general secretary.  Efforts to get comments from Suliman Otieno Owuor as well as from Salim Kumaka who is in management were futile as our calls went unanswered. We managed to obtain the DWU constitution which states that for one to vie for the position of general secretary one must be an outsider and that it is mandatory for any employee to resign with prior notice to the management.  Abubakar has intensified his campaigns by traversing the estates to woo for votes ahead of the August 13 poll. He is among those dismissed from employment at the Kenya Ports Authority (KPA) alongside other union officials following an illegal strike during former KPA Managing Director the late Francis Gichiri Ndua's tenure as Managing Director under ...

KAUNTI YA KWALE KUJIUNGA NA KESI YA ARDHI YA MBUGUNI

Image
Serikali ya Kaunti ya Kwale imetangaza kuwa itajiunga kama mdau katika kesi inayoendelea mahakamani kuhusu umiliki wa ardhi ya Mpango wa Makazi wa Mbuguni, Wadi ya Tsimba Golini, Kaunti Ndogo ya Matuga, ili kutetea haki za wakazi wanaopinga utoaji unaodaiwa kuwa kinyume cha sheria wa hati miliki. Hatua hiyo imetangazwa na Gavana Fatuma Achani baada ya wakazi kulalamikia kile walichodai kuwa baadhi ya hati miliki zilitolewa kwa watu wasiokuwa wenyeji wa eneo hilo pamoja na watu wenye ushawishi, hali iliyozua hofu ya kupokonywa ardhi wanayoitegemea kwa makazi na shughuli za kujipatia riziki. Mpango wa Makazi wa Mbuguni una takriban vipande 756 vya ardhi vilivyo katika vijiji vya Bang'a, Mteza, Mrera, Mbuguni na Lunguma. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mbuguni kujadili mzozo huo, Gavana Achani alisema serikali yake haitavumilia unyakuzi wa ardhi na imejizatiti kushirikiana na timu ya mawakili wa wakazi kuhakikisha haki inatendeka. "Serika...

KAMPENI ZAPAMBA MOTO KABLA YA UCHAGUZI WA CHAMA CHA WAFANYAKAZI WA BANDARINI

Image
MWANAHABARI: SHOKAH JUMA Kampeni za uchaguzi wa viongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Bandarini (DWU) zimeanza kushika kasi huku wanachama wakijiandaa kwa uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Agosti 13 mwaka huu.  Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Abubakar Mohammed Abdullahi, ameanza rasmi kampeni zake na kwa sasa ndiye mgombea pekee ambaye ametangaza nia ya kuwania wadhifa wa Katibu Mkuu, nafasi iliyoachwa wazi kufuatia kubatilishwa kwa uchaguzi wa awali.  Abubakar amekuwa akifanya mikutano katika maeneo mbalimbali ya makazi ya wafanyakazi wa bandarini akiwashawishi wanachama kumpigia kura siku ya uchaguzi. Katiba ya DWU inaeleza kuwa anayewania nafasi ya Katibu Mkuu lazima awe mtu wa nje ya ajira ya chama, huku mfanyakazi yeyote anayenuia kugombea akitakiwa kujiuzulu kazi kwa kutoa notisi kwa mwajiri wake.  Jitihada za kupata maoni kutoka kwa Suliman Otieno Owuor na Salim Kumaka hazikufanikiwa baada ya simu zetu kutopokelewa.  Abubakar ni miongo...

Kilimo Himilivu Chabadilisha Maisha ya Wakulima Kinango

Image
Na Jumwa Mwandoro  Kwa miaka mingi, eneo la Kinango, Kaunti ya Kwale, limekuwa likitajwa kama mojawapo ya maeneo yanayokumbwa na ukame wa mara kwa mara, hali iliyosababisha uhaba wa chakula na changamoto za kiuchumi kwa wakazi wake. Hata hivyo, juhudi za Shirika la Climate Care zinaanza kubadilisha taswira hiyo kupitia miradi ya kilimo himilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi. Kupitia mradi wa "Sikiliza Sauti, Dunia Inaita" , unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Shirika la WeWorld , Climate Care linafundisha zaidi ya makundi 20 ya wanawake na vijana yameanza kunufaika na mafunzo yanayolenga kuboresha mbinu za kilimo na kuimarisha usalama wa chakula. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Climate Care, Peter Tsuma , alisema lengo kuu la mradi huo ni kuwajengea wakulima uwezo wa kutumia mbinu za kisasa na rafiki kwa mazingira ili kuongeza uzalishaji wa mazao licha ya athari za mabadiliko ya tabianchi. "Makundi ...