Posts

SEKTA YA UVUVI KWALE YAPIGWA JEKI

Image
msafara wa naibu gavana na maafisa wa EU  KEMFSED na waziri Kilimo, Uvuvi na ufugaji      Taarifa yake : Caroline Katana  Sekta  ya uvuvi kaunti ya Kwale inatarajiwa kuimarika hata zaidi baada ya  makundi ya wasimamizi wa bahari  ( Beach Management Units ) kupokea boti  nane za kisasa chini ya ufadhili wa Jumuiya ya Ulaya EU kupitia mradi wa Go- Blue na serikali ya kaunti kupitia mradi wa KEMFSED  . Boti tano zilizofadhiliwa na EU zitawafaidi wavuvi kutoka eneo la Shimoni , Kibuyuni na Mkwiro huko boti  tatu za  ulinzi  ( patrol boats )  zilizofadhiliwa na serikali ya Kwale kupitia mradi wa KEMFSED zitatumika  na wavuvi katika sehemu za ushirika za Shimoni –Vanga, Mwandamu- Funzi  na Chale- Gazi. boti za Uvuvi kwale shimoni Zaidi ya wakaazi elfu kumi  kusini mwa pwani  wanategemea bahari moja kwa moja  kujikimu kimaisha . Nchini kenya ,uvuvi unajumuisha Zaidi maji chumvi ( maziwa ,mito na mabw...

WAAMUZI WA KIKE KWALE ON 4TH OCT 2024 LEO TV

Image
Idadi ya marefa wa kike wanaosimamia mechi za ligi za shirikisho la kandanda nchini (FKF) kaunti ya kwale inaendelea kuongezeka baada ya akina dada 8 kufuzu. Wanane hao wakiwa ni miungoni mwa wengine 26 ambao wamepokea ufadhili huo kupitia shirika la samba sports youth agenda na kampuni ya uchimbaji madini ya base titanium kutoka kaunti ya kwale.  Ongezeko hilo la waamuzi wakike ni mikakati ilowekwa na shirikisho la kandanda ulimwenguni kufikia elfu 2 na 32 timu za wanawake zi simamiwe na wanawake wenyewe.

IDADI YA REFARII /WAAMUZI WAKIKE WANAOFUZU KILA MWAKA YAONGEZEKA KWALE.

Image
Waamuzi wakike katikati ya uwanja na pembeni. Taarifa yake : Caroline Katana  Katika soka  refarii anakuwa na nafasi kubwa sana ya kuufanya mchezo  wa soka kuwa mzuri au kuuharibu. Katika  soka refarii anakuwa na kazi ya kusimamia sheria za mchezo  wa soka na kama  muamuzi wa mwisho  katika mechi , refarii  ndio  ana uwezo  wa kuamuru pambano liendelee au lisiendelee. Jumapili  iliyopita  waamuzi wa kike wanane kati ya waamuzi 26 walifuzu  kuchezesha timu  mbalimbali za soka kaunti ya Kwale na hata  ligi za  taifa. Mafunzo hayo yalitolewa na shirika la Sambasports Youth Agenda  kwa ushirikiano na usimamizi wa kampuni ya uchimbaji madini  ya Basetitanium  na shirikisho la soka la FKF tawi la Kwale. Idadi ya  waamuzi wa kike inaongezeka  pia ,mwaka wa  2013 refarii  wakike  watano  walifuzu kati  ya refarii ishirini na nne  waliopokea mafunzo hayo. Ubaguzi...

WASHUKIWA 26 WA UHALIFU WAKAMATWA DIANI.

Image
Maafisa wa usalama Msambweni  Taarifa yake : Caroline Katana Washukiwa 26 wa uhalifu waliokuwa wamejihami kwa mapanga wanazuiliwa katika kituo cha polisi cha Diani kaunti ya Kwale baada ya kukamatwa katika oparesheni ya pamoja iliyofanywa na asasi za usalama eneo la Msambweni usiku wa Jumanne. Vijana hao wenye kati ya umri wa miaka 14 hadi 21 wanadaiwa kuwahangaisha wenyeji kwa kuwakatakata mapanga kabla ya kuwaibia mali zao. Washukiwa hao ambao ni miongoni mwa magenge ya wahalifu yanayosakwa na polisi wamekamatwa katika eneo la Kibundani ,Kona ya Musa ,Ibiza na Bongwe. Mwenyekiti wa kamati ya usalama ambae pia ni naibu kamishna eneo la Msambweni Josphat Mutisya amesema kuwa washukiwa hao walikwepa mkono wa sheria siku ya Jumapili baada ya kuwajeruhi wakaazi muda mfupi baada ya kukamilika kwa mchezo wa soka katika uwanja wa Shamu. “ Maafisa wa polisi walipata hizo habari wakafika katika eneo la tukio lakini hawakufaulu kuwakamata ,mikakati ya msako wa pamoja iliafikiwa na usiku wa ...

UKATILI WA WAZAZI KWALE

Image
Johnstone Kivuli afisa wa maswala ya watoto Msambweni.  Taarifa yake : Caroline Katana Wizara ya watoto kaunti ya Kwale imekemea vikali vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto na baba zao wakati wazazi wao wakike wanaposafiri mataifa ya nje kutafuta ajira. Hii ni baada ya afisi hio kuanza kurekodi idadi ya juu ya kesi hizo za watoto waliochiwa wazazi wa kiume kupitia dhulma za kingono. Afisa wa watoto eneo bunge la Msambweni Jonstone Kivuli akielezea kusitikishwa kwake na jinsi watoto wachanga wanavyodhulumiwa haki zao na watu wanaofaa kulinda haki zao. “ Kwa sasa hivi nashughulikia kesi mbili mahakamani za watoto waliodhulumiwa kingono na baba zao ,hizi ni kesi ambazo awali hazikuwa zinasikika lakini kwa sasa hivi tumeona hizi kesi zikiripotiwa kwa wingi katika afisi zetu ,” Asema bw.Kivuli. Utafiti uliofanywa na Kenya Demographic and Health Survey KDHS 2022 unaonyesha asilimia 14.8% ya wasichana wenye umri wa miaka 15-19 kaunti ya Kwale wamewahi kupata mimba idadi iliyotajwa ku...

UFISADI KATIKA SERIKALI ZA KAUNTI UMESAMBARATISHA HUDUMA ZA MAJI KWA WANANCHI

Image
Watetezi wa haki ya maji na usafi wa mazingira nchini. Taarifa yake : Caroline Katana Afya bora ,maji safi na salama ni mahitaji msingi ya binadamu ,lakini pia yana umuhimu wake kwa viumbe wote wanaoishi duniani. Walimwengu wanapaswa kufaidika na haki hii msingi katika maisha yao . Uhaba wa maji safi na salama unaweza kuwa chanzo cha migogoro kinzani kwa siku za usoni ikiwa kama serikali ya kitaifa na zile za kaunti hazitasimama kidete kulinda vyanzo vya maji pamoja na kutambua kwamba maji ni sehemu ya haki msingi za binadamu. Huduma bora za maji safi na salama ni kichocheo kikuu cha maisha na afya bora Zaidi. Dhana ya maji kuwa ni sehemu ya haki msingi za binadamu ni agenda iliyoibuliwa hivi karibuni ,lakini inaendelea kushika kasi kubwa sana katika jumuiya ya kimataifa kutokana na unyetiwake. Ndio maana kuna haja ya kuwa na miundo mbinu ya kisheria ,kiufundi ,kijamii na kisiasa ili kuanzisha mchakato wa ujenzi wa utamaduni wa utunzaji bora wa vyanzo vya maji. Maji ni muhimu sana kwa ...

KANDANDA YA HAKI KWA MTOTO WA KIKE KWALE.

Image
SHE LEADS TIMU KWALE. Taarifa yake : Caroline Katana Lengo la michezo hususan kandanda si kushinda pekee ,inaweza kuunganisha au kuwatenganisha watu kulingana na jinsi itakavyotumiwa , Kwa mujibu huu,makocha wana wajibu mkuu katika maisha ya wachezaji wachanga hususani watoto wakike. Si kuwatayarisha tu kwa kandanda ya malipo bali wanastahili kuwa wazazi, rafiki, walinzi, vilelezo washauri na watu wa kuigwa na wachezaji. Wasiwafunze tu jinsi ya kufanikiwa katika Michezo bali pia katika maisha kwa kuzingatia dhana ya “Michezo kwa Maendeleo” Vijana wachanga wanahitaji kupata mafunzo ya hali ya juu kisaikolojia na kimichezo ili waweze kuepuka vishawishi potofu vinavyolenga kusambaratisha maisha yao. Shirika la Network for Adolescent youth of Africa NAYA linaendeleza mchakato wa kuwawezesha vijana wakike katika maswala ya utetezi na uongozi ili waweze kutambua haki zao katika jamii. TIMU YA WANAWAKE SHE LEADS KWALE. NAYA ikitekeleza juhudi hizi kupitia kandakanda na vikao vya hamasa vijiji...

RIPOTI YA UTAFITI WA ELIMU ENEO LA PWANI YAZINDULIWA RASMI NA SHIRIKA LISILOKUWA LA KISERIKALI LA USAWA AGENDA.

Image
Uzinduzi wa ripoti ya FLANA. Taarifa yake : Caroline Katana. Shirika lisilokuwa la kiserikali la Usawa Agenda kwa ushirikiano na mashirika mbalimbali ya kijamii ukunda wa pwani yamezindua ripoti maalum inayofahamika kama Foundation Literacy and Numeracy Assessment FLANA yenye tathmini ya viwango vya elimu eneo la pwani. Hii baada ya utafiti uliofanywa katika kaunti zote 47 nchini mwaka uliopita ili kutathmini viwango vya kusoma ,kuandika na kuhesabu miongoni mwa watoto wenye umri wa miaka kati ya 6 -16 ili kuchochea sera zenye ushahidi ambazo zingeweza kusababisha ujifunzaji sawa kwa watoto wote. mratibu wa shirika la Usawa Agenda kaunti ya Kwale Amani Lugogo Mratibu wa shirika la Usawa Agenda kaunti ya Kwale ambaye pia ni mwanachama wa shirika la kijamii la Kwale Youth and Governance Consortium KYGC Amani Lugogo amesema kuwa utafiti huo ulijumuisha vijiji 230 ,nyumba 6,348 , watoto 3,016 na shule 226 ukunda wa pwani. “ Leo hii tuko hapa kuzindua ripoti ya elimu ya pwani ambapo kaunti ...

SS ASSAD FC INATARAJIWA KUNG’AA KATIKA MICHUANO YA FKF NATIONAL SUPER LEAGUE 2024/2025.

Image
SS ASAD KWALE Taarifa yake : Caroline Katana Bodi simamizi ya timu ya soka ya SS ASSAD FC imeelezea matumaini yake ya timu hio kuibuka na ushindi katika michuano ya FKF National Super League 2024/2025 inayotarajiwa kuanza rasmi tarehe 7 mwezi huu . Raisi wa SS Assad Richard Onsongo aliyekuwa akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa vifaa vya michezo vya timu hio vilivyofadhiliwa na serikali ya kaunti ya Kwale vyenye gharama ya shilingi Milioni 2 iliofanyika katika uwanja wa maonyesho wa Ukunda show ground ,amesema kuwa malengo yao ni kuona timu ya SS Assad ikipata ushindi na kuingia katika michuano ya Premier League. Raisi wa klabu  cha SS Assad Richard Onsongo. Onsongo aidha akiafiki awali timu ya SS Assad kukumbwa na changamoto ya uongozi hatua ambayo ilipelekea timu hio kushuka kwa kiwango kikubwa . “ Msimu uliopita kumekuwa na changamoto msingi zilizokumba vijana wetu kufuatia uongozi mbaya wa bodi iliyopita ,lakini msimu huu tunatarajia ushindi baada ya kuteuliwa kwa bodi mpya ...

USIMAMIZI WA BASETITANIUM WAJITENGA NA MADAI YA KUAHIDI KULIPA MILLION 7 KWA SHIRIKA LA KIJAMII LA SPORTS FOR ALL

Image
wafanyikazi wa shirika la kijamii la sports for all Usimamizi wa kampuni ya uchimbaji madini ya basetitanium umejitenga na madai ya kueneza ukabila ,ahadi za uongo na utumizi mbaya wa afisi yaliyoibuliwa na shirika la kijamii la michezo la Sports For All, ukiyataja madai hayo kukosa msingi na yanalenga kudhalilisha usiamamizi wa kampuni hio wakati inapojiandaa kufunga virago vyake mwishoni mwa mwaka huu . Wafanyikazi wa Shirika la sports for all wanalalamikia kutolipwa mishahara yao ya miezi mitatu ya shilingi milioni 3 ya mwaka 2018 mbali na shilingi milioni 7 ya mkataba wao uliokamilika mwezi June. wafanyikazi wa shirika la kijamii la sports for all Kadhalka wakidai kuwa usimamizi wa basetitanium umedinda kuwapa vifaa walivyokuwa wakifanyia kazi ikiwemo laptops ,printers ,files miongoni mwa vifaa vyenginezo. Wanaitaja hatua hio kukiuka haki zao ,hivyo kutaka usimamizi wa basetitanium kutimiza ahadi zao ikizingatiwa kuwa wamefanya kazi kwa ushirikiano kwa muda wa miaka kumi sasa. Mane...